Psalms 96

Mungu Mfalme Mkuu

(1 Nyakati 16:23-33)


1 aMwimbieni Bwana wimbo mpya;
mwimbieni Bwana dunia yote.

2 bMwimbieni Bwana, lisifuni jina lake;
tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.

3 cTangazeni utukufu wake katikati ya mataifa,
matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.


4 dKwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote;
yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.

5 eKwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu,
lakini Bwana aliziumba mbingu.

6 fFahari na enzi viko mbele yake;
nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.


7 gMpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa,
mpeni Bwana utukufu na nguvu.

8 hMpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake;
leteni sadaka na mje katika nyua zake.

9 iMwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake;
dunia yote na itetemeke mbele zake.


10 jKatikati ya mataifa semeni, “Bwana anatawala.”
Ulimwengu ameuweka imara, hauwezi kusogezwa;
atawahukumu watu kwa uadilifu.

11 kMbingu na zishangilie, nchi na ifurahi;
bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;

12 lmashamba na yashangilie,
pamoja na vyote vilivyomo ndani yake.
Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha;

13 mitaimba mbele za Bwana kwa maana anakuja,
anakuja kuihukumu dunia.
Ataihukumu dunia kwa haki,
na mataifa katika kweli yake.
Copyright information for SwhKC